Afisa mmoja wa Umoja wa Falme za Kiarabu UAE amesema, meli ya mafuta MT Riah iliyoripotiwa kupotea haimilikiwi na kuendeshwa na nchi hiyo. Kwa mujibu wa shirika la habari la nchi hiyo WAM, afisa huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema meli hiyo haikuwabeba wafanyakazi wa UAE wala kuomba msaada. Vyombo vya habari vya kimataifa vinasema meli hiyo ya mafuta iliyopeperusha bendera ya Panama ilipotea ilipokuwa ikipita mlango bahari wa Hormuz.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |