Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi 14 wanachama wa Umoja wa Ulaya zimekubaliana kuwa na mfumo mpya wa mshikamano ili kuwapatia makazi wahamiaji katika eneo hilo, zikiahidi kutafuta juhudi zaidi za kidiplomasia ili kuunga mkono zaidi pendekezo la Ujerumani na Uingereza kuhusu uhamiaji.
Rais Macron amesema hayo alipokutana na waandishi wa habari baada ya mkutano kati yake na Kamishna wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Uhamiaji Bw. Filippo Grandi na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji Bw. Antonio Vitorini mjini Paris. Amesema kati ya nchi hizo 14, nchi nane zimethibitisha ushirikiano wao na kuhusika kwao katika mfumo huo wa mshikamano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |