Serikali imetoa onyo kali kwa wafanyibiashara na mashirika yanayokwepa kulipa ushuru. Wizara ya hazina ya kitaifa imependekeza kufutiliwa mbali kwa leseni za utendakazi za wafanyibiashara na mashirika yote ambayo yamekuwa yakikwepa kulipa ushuru. Takriban shilingi bilioni moja za ushuru zilirejeshwa kutoka kwa kampuni kadhaa zilizokuwa zimehepa kulipa ushuru. Aidha kampuni 2,000 nchini Uganda zinafanyiwa uchunguzi kuhusiana na swala la kutolipa ushuru kwa URA.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |