Aliyekuwa waziri wa mambo ya nje na meya wa zamani wa London Bw Boris Johnson, leo amechaguliwa kuwa kiongozi wa chama tawala cha wahafidhiana na kutarajiwa kuwa waziri mkuu wa Uingereza.
Bw. Johnson amepata kura 92,153 dhidi ya 46,656 alizopata mpinzani wake ambaye ni waziri wa mambo ya nje wa sasa Bw. Jeremy Hunt.
Baada ya matokeo hayo kutolewa, Johnson amesema akiwa waziri mkuu ataleta "moyo mpya wa mambo ya kuweza kufanya".
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |