Wanamaji kutoka meli ya mafuta ya NEYMA ya Russia walioshikiliwa na Idara ya usalama ya Ukraine wameachiliwa. Wakati huohuo, wanamaji hao wanapaswa kufanyiwa mahojiano ya simu na wapelelezi, ambayo haviwazuii kusafiri na wanaweza kuondoka nchini humo. Awali, Idara ya usalama ya Ukraine na Ofisi ya uendeshaji mashtaka ya Jeshi zilikamata meli hiyo katika bandari ya Izmail ya Ukraine kutokana na kuhusika na tukio la Ushoroba wa Kerch.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |