Onyo hilo lilitolewa na Naibu Waziri wa Kilimo, Omary Mgumba, baada ya kutembelea na kujionea pamba ikiwa imehifadhiwa nje ya ghala katika chama cha msingi cha ushirika (Amcos) Zuya Mtaa wa Nyakabindi Halmashauri ya Mji Bariadi.
Mgumba alisema wanunuzi wa pamba walikubaliana na serikali wadhaminiwe ili kukopeshwa na benki, jambo ambalo lilifanyika, lakini anashangaa kwa nini mpaka leo wameshindwa kununua pamba.
Alisema serikali ilichukua dhamana hiyo kwa ajili ya kuwasaidia wakulima wa pamba na fedha ambazo wanunuzi walikopeshwa na benki zinatakiwa kutumika kwa ajili ya kununua pamba tu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |