Kiongozi wa Korea Kaskazini Bw. Kim Jong-un amepongeza majaribio ya kombora jipya ambayo yamefuatiliwa sana na Korea Kusini na Marekani.
Habari kutoka Korea Kaskazini zinasema Bw. Kim Jong-un amesisitiza kuwa, anatarajia serikali ya Korea Kusini itatambua hatari ya mustakabali wa hali iliyopo, kusimamisha kuingiza silaha za kisasa na kufanya mazoezi ya kijeshi, na kurudi kwenye makubaliano yaliyofikiwa mwezi wa Aprili na Septemba, mwaka jana. Habari zinasema, Marekani na Korea Kusini zimeona kitendo hicho cha Korea Kaskazini hakitasaidia kutuliza hali ya mvutano wa peninsula ya Korea, na kuihimiza Korea Kaskazini kufuata maazimio husika ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |