Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bibi Hua Chunying leo amesisitiza katika mkutano na waandishi wa habari kuwa, serikali kuu ya China inaiunga mkono serikali ya eneo maalum la Hongkong kuchukua hatua kulinda utulivu, usalama na ustawi wa Hongkong. Amesema kikosi cha ulinzi cha jeshi la China mkoani Hongkong kinafuata sheria ya kimsingi ya Hongkong na sheria ya jeshi la ulinzi ya Hongkong, na kimekuwa uhakikisho wa ustawi na utulivu wa kudumu wa Hongkong.
Pia Bibi Hua Chunying alisisitiza kuwa, Hongkong imeendelea kwa utulivu na ustawi katika miaka 22 iliyopita chini ya uungaji mkono wa serikali kuu ya China. Amesema Hongkong ni sehemu ya China na China hairuhusu nguvu yoyote ya nchi za nje kuingilia kati ya mambo ya sehemu hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |