Dili jipya limefanyika Milwaukee Bucks ambayo imemtoa Thanasis Antetokounmpo nchini Ugiriki akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na timu ya ligi ya kikapu ya nchini kwao. Meneja wa Bucks, Jon Horst amemtangaza mchezaji huyo kuwa ataongeza nguvu kwenye timu hiyo kulingana na alichokitaja kuwa mzoefu na mwenye uwezo wa kushindana. Thanasisi ataungana na kaka yake Giannis ambaye ni MVP wa msimu uliopita kukipiga katika timu hiyo ya Milwaukee Bucks.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |