Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema usajili wa Elliot ndani ya klabu yake ni muhimu sana na wenye manufaa. Amebainisha lengo la kuwasajili vijana ndani ya Anfield ni kuwakuza ili baadaye wawe na makali ya kutosha.
Elliot mwenye miaka 16 alicheza mchezo wa ligi kuu akiwa amevaa uzi wa Fulham katika mchezo dhidi ya Wolverhamton, na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji mwenye umri mdogo kabisa kupata kucheza ligi kuu ya Uingereza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |