Watanzania wamehimizwa kutumia maonyesho ya tarehe nane mwezi wa nane, almaarufu nane nane ya mwaka huu, kusajili biahsra zao. Hii ni pamoja na majina ya biashara, kampuni, alama za biashara pamoja na leseni za viwanda na za biashara.
Wito huu umetolewa na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela), Emmanuel Kakwezi. Maonyesho hayo yatakayofanyika mkoani Simiyu, Brela pia itasajili leseni za usafirishaji wa mifugo na mazao ya chakula ndani nan je ya nchi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |