Serikali imeombwa kuzidi kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kuwavutia wawekezaji wengi wa ndani na nje hapa nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari hiyo jana, katika mkutano ulioandaliwa na Chama wa Waajiri Tanzania (ATE), Mkurugenzi Mtendaji, Dk. Aggrey Mlimuka amesema endapo Watanzania na wawekezaji wageni watawekeza biashara endelevu itazidi kuchagiza kwa kasi ya ukuaji wa uchumi nchini.
Amesema uwekezaji wa China ni mkubwa na wenye tija kwa Tanzania kwa sababu unaongeza ajira na viwanda nchini humo. Kufanikisha hili, lazima mazingira ya kufanyia biashara yawe salama nay a kuvutia wawekezaji zaidi.
Katika mkutano huo ulioandaliwa na ATE umeshirikisha wawekezaji toka nchini Norway na China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |