Sherehe za ufunguzi zimeshuhudia kupandishwa bendera tatu na mwanariadha nguli David Rudisha na mkuu wa hoteli hiyo yenye matawi mbalimbali.
Hoteli hiyo ambayo imekuwa ikikarabatiwa inamilikiwa na raia wa Thailand ilisalia imefungwa tangu tukio la shambulizi la kigaidi ambalo kundi la al-Shabaab lilikiri kuhusika.
Hoteli hiyo ambayo imekodisha asilimia kubwa ya vyumba vilivyoko 14 Riverside Complex ilisalia imefungwa licha ya afisi za biashara nyinginezo kufunguliwa.
Wateja walianza kupata huduma katika hoteli hiyo siku ya Alhamisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |