Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinajitahidi kuunganisha mfumo wa malipo ya elektroniki wa kikanda na suluhisho zingine za malipo barani Afrika, ili kurahisha biashara kote barani Afrika kufuatia uzinduzi wa eneo la Biashara Huria la Bara la Afrika (AfCFTA).
Benki kuu za EAC sasa zinachunguza njia za kubadilisha mfumo huo kwa kuiunganisha na suluhisho zingine za malipo barani Afrika kuwezesha utumaji wa pesa taslimu katika bara zima kwa viwango vya rejareja na vya jumla.
Naibu gavana wa Benk Kuu ya Uganda Dk. Louis Kasekende amesema hatua hiyo itasaidia kukuza biashara ya ndani ya Afrika na kuunga mkono ukuaji wa mashirika ya kikanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |