Jeshi la Syria limetangaza kuanzisha tena operesheni za kijeshi mkoani Idlib, kaskazini magharibi mwa nchi hiyo, kutokana na vikosi vya upinzani kukataa makubaliano ya kusitisha vita na kufanya mashambulizi kadhaa dhidi ya raia.
Taarifa iliyotolewa na jeshi hilo pia imeilaumu Uturuki kwa kupuuza wajibu wake kutokana na makubaliano yaliyofikiwa awali kuhusu eneo la Idlib, na kuviruhusu vikosi vya upinzani vinavyoungwa mkono na nchi hiyo kufanya mashambulizi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |