Waziri wa mambo ya nje wa Iran Bw. Mohammad Javad Zarif amesema mauzo ya mafuta ya Iran kwa nje yanatakiwa yasipungue mapipa milioni 2.8 kwa siku chini ya Makubaliano ya nyuklia ya Iran JCPOA yaliyofikiwa mwaka 2015.
Amesema matakwa hayo yamewasilishwa kwa nchi za Ulaya zilizosaini makubaliano hayo, na kwamba mauzo ya mafuta ya Iran kwa nje yanapaswa kurejeshwa hadi kufikia kiwango cha mwezi Mei mwaka 2018 wakati Marekani ilipojitoa kwenye makubaliano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |