Mamlaka ya kuratibu umeme nchini Uganda REA imesema kuwa itapunguza kwa asilimia 50 ada inayotozwa taa za barabarani.
Mamlaka hiyo imesema punguzo hilo litatekelezwa hadi mwezi Septemba na sasa malipo mapya ni shilingi 371 ikilinganishwa na malipo ya awali ya 742.
Mkurungezi wa mawasiliano wa mamlaka Julius Wandera, amesema punguzo hilo linalenga kuimarisha usalam katika mjini yote kote nchini humo.
Hatua hii pia ni baada ya serikali kupunguza malipo ya umeme kwa viwanga hadi cneti 8 wakati wa masaa ya ziada.
Zaidi ya asilimia 70 ya umeme wa Uganda hutumiwa na viwanda chini ya chama cha watengenezaji bidhaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |