Rais Donald Trump wa Marekani alisaini amri ya kuzuia mali zote za serikali ya Venezuela nchini Marekani, mali hizo haziwezi kutumika kwa njia za kukabidhi, kulipa na uuzaji bidhaa kwa nchi za nje. Aidha raia wa Venezuela wanaofanya kazi kwenye serikali ya Venezuela huenda watapigwa marufuku kuingia Marekani.
Serikali ya Venezuela imelaani vikali amri hiyo na kusema vikwazo hivyo ni ugaidi wa kiuchumi na vitaathiri vibaya uchumi na jamii ya Venezuela, pia ni kitendo cha kipuuzi na aibu kubwa kabisa cha uporaji katika historia ya uhusiano wa kimataifa katika karne za hivi karibuni. Imesema raia wote wa Venezuela watashikamana kupambana na ugaidi wa kiuchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |