Shirika la ndege la Uganda linatarajiwa kuanza upya safari zake Agosti 28 kwenda kwenye miji ya kikanda.
Shirika hilo halijakuwa likihudumu kwa miaka 20.
Safari za kwanza zitakuwa kati ya Entebbe, Nairobi na Juba mara mbili kwa wiki, mara moja kwenda Dar es Salam na nne Mogadishu.
Shirkka hilo lilinunua ndege 4 aina ya Bombardier CRJ na mbili ziliwasili mwezi Aprili huku nyingine mbili zikitarajiwa kuwasili mwezi Septemba.
Mipango yake ya baadaye ni kuongeza safari zake kwenye Bujumbura Mombasa na Kilimanjaro.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |