Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Bw. Mevlut Cavusoglu amesema makubaliano kati ya nchi hiyo na Marekani kuhusu kuanzisha eneo salama kaskazini mashariki mwa Syria ni mwanzo mzuri.
Jumatano wiki hii, Uturuki na Marekani zilifikia mwafaka wa kuanzisha kituo cha operesheni za pamoja nchini Uturuki ili kuratibu na kusimamia eneo salama lililopangwa kuanzishwa nchini Syria, hatua inayotarajiwa kupunguza uwezekano wa uingiliaji wa kijeshi wa Uturuki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |