Kampuni hiyo imesema hasara hiyo ni mara 7 ya ile iliopata kipindi sawa na hicho mwaka jana.
Mauzo yake ya hadi mwishoni mwa Juni yalifikia milioni 29 iliwa ni upungufu wa kutoka milioni 42 mwaka 2018.
Mwenyekiti wa kampuni hiyo Richard Korir amesema kudorora kwa mapato kumechangiwa na kushuka kwa bei ya chai kwenye soko la kimataifa.
Kampuni nyingine za chai pia zimetumbukia kwenye hasara huku ile ya Eaagads tayari ikitoa taarifa ya kuwa na uwezekano wa hasara.
Sasini Tea ilipata hasara ya shilingi milioni 194 katika kipindi kilichokamilika machi 2019.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |