Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema usalama wa usafiri wa meli katika eneo la Ghuba ya Uajemi unapaswa kulindwa na nchi zinazopakana nayo kwa pamoja, na anapinga kithabiti uingiliaji wa nje. Rais Rouhani amesema hayo kwenye mkutano wa Baraza la Mawaziri baada ya Marekani hivi karibuni kutaka washirika wake kujiunga na "muungano wa kulinda usafiri" katika eneo la Ghuba ya Uajemi. Wachambuzi wanasema Marekani inalenga kuchochea "tishio la Iran" na kuongeza shinikizo kwa nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |