• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mauzo ya nje ya Rwanda yaongezeka kwa asilimia 7.5

    (GMT+08:00) 2019-08-15 18:25:05
    Mauzo ya nje ya Rwanda yameongezeka katika nusu ya mwaka huu,yakichangiwa na mauzo ambayo haiuzi nje mara kwa mara licha ya kushuka kwa bei ya bidhaa katika soko la kimataifa.

    Kulingana na data za Benki Kuu ya Rwanda ambazo zilitolewa jana,mauzo ya nje yaliongezeka kwa asilimia 7.5 na bidhaa ambazo Rwanda iliagiza kutoka nje ziliongezeka kwa asilimia 18,na kusababisha nakisi kubwa ya biashara.

    Gavana wa Benki ya Rwanda John Rwangombwa alisema bidhaa ambazo kwa kawaida huuzwa sana nje kama vile madini,chai na kahawa hazikufanya vizuri lakini wamepata utendaji mzuri katika bidhaa ambazo sio kawaida kuuzwa nje haswa zile zilizoundwa Rwanda.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako