Waziri wa ulinzi wa Russia Sergei Shoigu na mwenzake wa Venezuela Vladimir Padrimo Lopez wamesaini makubaliano ya kutembeleana kwa manowari za kijeshi katika bandari za nchi hizo mbili. Katika mkutano wao uliofanyika mjini Moscow, mawaziri hao pia wamejadili hali ya Venezuela na masuala ya ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili. Bw. Padrino Lopez amesema Marekani imekiuka vikali sheria ya kimataifa katika jaribio lake la kupindua serikali halali ya Venezuela.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |