• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Zanzibar yapigia debe utalii wa majahazi

    (GMT+08:00) 2019-08-16 18:58:24
    Waziri wa habari, utalii na utamaduni wa Tanzania Bw Mahmoud Thabit Kombo, amesema utalii wa majahazi ni kivutio kikubwa cha watalii licha ya kwamba Zanzibar inapokea watalii wengi wanaosafiri kwa kutumia ndege.

    Aliyasema hayo wakati akizungumza katika hafla ya kumuaga Nassir Salum Mabrouk ambaye atashiriki tamasha la safari ndefu duniani kwa kutumia usafiri wa boti katika kutembea dunia nzima kupitia baharini.

    Alimtaka mshiriki huyo ambaye ni pekee kwa nchi za Afrika Mashariki kuitangaza Zanzibar kiutalii kupitia mashindano hayo.

    Kombo alisema iko haja ya kukuza utalii wa bahari ili watalii wanaofika Zanzibar watumie usafiri wa baharini.

    Mashindano hayo ya tamasha la safari ndefu duniani, hutumia boti ambayo haitumii mashine na badala yake itakua inategemea upepo na watazunguka mabara sita.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako