Waziri anayeshughulikia Brexit Bw. Stephen Barclay amesaini amri itakayofuta sheria zote za Umoja wa Ulaya zinazotumika nchini Uingereza kuanzia Oktoba Mosi mwaka huu.
Taarifa iliyotolewa na serikali ya Uingereza imesema, Barlclay amesaini sheria ya kufuta Azimio la Bunge lililokubali nchi hiyo kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya (EEC) mwaka 1972.
Amri hiyo itafuta Azimio hilo la mwaka 1972, na kutekeleza kihalisi Mkataba wa Uingereza kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |