Idadi ya watu waliofariki dunia kufuatia mvua kubwa na mafuriko nchini Sudan imeongezeka hadi 62. Kaimu naibu waziri wa afya wa Sudan Bw. Sulaiman Abdul-Jabbar amesema, watu wengine 98 wamejeruhiwa, jumla ya familia 35,850 zimeathiriwa kote nchini na nyumba 22,676 zimeharibiwa kabisa. Hata hivyo amesema Sudan ina uwezo wa kukabiliana na hatari za msimu huu wa mvua.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |