Ubalozi wa Marekani nchini Sudan umetangza kutoa dola za kimarekani milioni 2 ili kuisaidia nchi hiyo kukabiliana na hali ya dharura inayotokana na mvua kubwa na mafuriko, huku Kuwait na Qatar nazo pia zikitangaza kutoa msaada wa kibinadamu kwa watu walioathiriwa. Kwa mujibu wa kaimu naibu waziri wa afya wa Sudan Sulaiman Abdul-Jabbar, watu 62 wamefariki na wengine 98 kujeruhiwa kutokana na maafa hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |