Rais Vladimir Putin wa Russia na mwenzake wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan wamesema nchi zao ziko tayari kupanua ushirikiano wa kijeshi. Rais Putin amewaambia wanahabari baada ya mazungumzo yao kando ya Maonesho ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga MAKS, wametumia fursa ya ziara ya rais Erdogan kujadili miradi mizuri ya pamoja sio tu katika usafiri wa anga bali pia ushirikiano wa kiufundi wa kijeshi. Ameongeza kuwa Russia iko tayari kuwaalika marubani wa Uturuki kupanda ndege za kivita aina ya Su-30SM.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |