Wakicheza nyumbani baada ya kutoka sare tasa ugenini jijini Bujumbura, Gor Mahia walicheza mchezo wa kuelewana na hatimaye kupata ushindi huo mnono kupitia kwa mshambuliaji wao Nicholas Kipkurui aliyekuwa mwiba kwa kupiga hat trick.
Akifunguka baada ya mchezo huo, Pollack amesema kilichosaidia ushindi ni mazoezi mazuri ambayo wamekuwa wakiyafanya kwa wiki nzima. Gor Mahia sasa itakutana na USM Algeirs ya Algeria kati ya Septemba 13 hadi 15 kwenye raundi ya pili ya mchujo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |