Ndege za kivita za muungano wa jeshi linaloongozwa na Saudi Arabia zimeshambulia mara kadhaa uwanja wa ndege wa mji wa Sanaa, Yemen, ambao unakaliwa na waasi wa Houthi, saa moja tu baada ya waasi hao kurusha kombora dhidi ya uwanja wa ndege wa Abha wa Saudi Arabia. Ripoti iliyotolewa na televisheni ya al-Masirah inayoendeshwa na waasi wa Houthi zinasema, kombora hilo limelenga kituo cha operesheni za kijeshi na mabanda ya ndege.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |