Rais Donald Trump wa Marekani amesema nchi hiyo na kundi la Taliban la Afghanistan ziko karibu kufikia makubaliano ya kupunguza wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan hadi 8,600. Hata hivyo rais Trump amesema nchi yake itadumisha nguvu ya kijeshi nchini Afghanistan. Mwaka 2002, Marekani ilianzisha vita vya Afghanistan baada ya mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11, na kuondoa utawala wa Taliban unaoaminiwa kuunga mkono kundi la al-Qaeda. Hivi sasa bado kuna wanajeshi karibu elfu 14 wa Marekani nchini Afghanistan.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |