Kenya ambayo sasa inajivunia mataji matano ya wanawake ya African Games, pamoja na Cameroon zitawakilisha Bara la Afrika katika michuano hiyo ya dunia. Malkia Strikers itamenyana na Marekani (Septemba 14), Uholanzi (Septemba 15), Serbia (Septemba 16), Brazil (Septemba 18) na Argentina (Septemba 19) mjini Hamamatsu, na kisha Itaelekea mjini Sapporo kupepetana na Jamhuri ya Dominican (Septemba 22), Japan (Septemba 23) na Uchina (Septemba 24).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |