• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • FIFA yamfungia miezi mine mchezaji aliyekataa kuchezea timu iliyomsajili

    (GMT+08:00) 2019-09-02 08:48:47
    Mchezaji wa kimataifa wa Iran mwenye asili ya Sweden Saman Ghoddos, amefungiwa kucheza soka kwa muda wa miezi minne na Shirikisho la soka duniani (FIFA) kutokana na kushindwa kuheshimu makubaliano aliyofikia ya kujiunga na klabu ya SD Huesca.

    Huesca iliyopanda ligi kuu ya Uhispania (La Liga) inadai kuwa, walishafikia makubalinao ya kumnunua Ghoddos kutoka klabu yake ya Sweden na kwamba mchezaji huyo alishasaini mkataba.

    Kamati ya utatuzi migogoro ya FIFA imebaini kuwa klabu hiyo ya Uhispania ilikuwa sahihi, mbali na kumfungia Ghoddos, FIFA imemtaka pia mchezaji huyo kuilipa fidia klabu hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako