Waziri mkuu wa Israel Bw. Benjamin Netanyahu amesisitiza kuwa, nchi hiyo itayajumuisha makazi ya wayahudi yaliyojengwa kwenye ukingo wa magharibi wa Mto Jordan kuwa ardhi yake, kauli ambayo imepingwa vikali na Palestina.
Msemaji wa rais wa Palestina ametoa taarifa ikisema, serikali ya Israel inadai mara kwa mara kukalia makazi yaliyojengwa kiharamu katika ardhi zinazokaliwa, na kuendeleza sera yake ya makazi, hatua ambayo haitaleta amani, usalama na utulivu kati ya Palestina na Israel.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |