Serikali ya Ujerumani imetangaza kuwa, ikiwa sehemu ya mpango wa kuondoa matumizi ya makaa ya mawe, nchi hiyo inapanga kugharamia Euro bilioni 40 kwa ajili ya kuyabadilisha maeneo ya uzalishaji wa makaa ya mawe na kutimiza uchumi endelevu. Fedha hizo zitatumiwa katika maeneo mengi yakiwa ni pamoja na kuboresha mawasiliano mapana "Broadband", na miundo mbinu mingine pamoja na kufanya uvumbuzi na uendelezaji. Mswada kuhusu matumizi hayo ya fedha utapitishwa mwishoni mwa mwaka huu kwenye bunge la Ujerumani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |