Shirika la Rwanda RwandAir, limepata ongezeko la abiria wa kwenda Dubai kwa asilimia 17, na mizogo kwa asilimia 38 katika miezi 7 ya kwanza ya 2019,.
Mohammed Al Rais, Mkurugenzi Msaidizi wa kampuni ya Al Rais inayowakilisha shirika hilo huko Dubai
alisema hayo wakati wa ziara ya kibiashara nchini Rwanda.
Al Rais alisema kuwa mwaka wa 2018 shirika hilo lilikuwa na abiria 42,000 kutoka Dubai kwenda Kigali
Kati ya hao, 20, 000 walisafiri kati ya Januari hadi Julai 2018.
Kufikia Julai mwaka huu, idadi ya abiria ilikuwa imeongezeka hadi 240, 000, na mizigo kutoka tani 200 hadi 280.
Rwandair inahudumu kati ya Kigali na Dubai mara nne kwa wiki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |