Shirika la habari la Iran limemkariri kiongozi mkuu wa nchi hiyo Ali Khamenei akisema kuwa, Iran itaendelea kusimamisha utekelezaji wa makubaliano ya nyuklia. Pia amesema Iran itatangaza mapema hatua za kusimamisha utekelezaji wa makubailano hayo katika kipindi cha tatu. Akisisitiza kuwa hatua hizo mpya zitaleta athari muhimu.
Ofisa wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran aliwahi kusema kuwa, endapo nchi nyingine zinazohusika hazitekelezi wajibu ipasavyo, Iran ina uwezo wa kurejesha urutubishaji wa uranium ndani ya siku mbili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |