Serikali ya Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson inataka kutoa hoja kwa mara ya pili Jumatatu ijayo ya kuitisha uchaguzi mkuu.
Johnson anaamini kuwa kufanya uchaguzi mkuu katikati ya mwezi Oktoba kutawaruhusu wananchi wa Uingereza kuamua kama atakwenda Brussels, akiwa na tishio lake la kufikiwa ama kutofikiwa makubaliano, au kutandika njia kwa chama kikuu cha upinzani cha Leba kufanya mazungumzo ya kuahirisha Uingereza kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |