Meneja wa TRA mkoani wa Kilimanjaro, Gabriel Mwangosi, amesema kuwa ziko leseni ambazo zilitelekezwa au kuachwa kwa muda mrefu hadi muda wake wa matumizi kwisha na maofisa wake kulazimika kuziteketeza kwa kuzichoma moto.
Mwangosi alisema hayo baada ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Anna Mghwira, kwenda kukagua shughuli zinaziofanywa na maofisa wa TRA na kuzungumza nao kuhusu mambo mbalimbali.
Kwa nyakati tofauti, baadhi ya watu wanaoomba leseni katika mamlaka hiyo, wamekuwa wakilalamikia kucheleweshwa kwa leseni hizo wakidai kwamba wanaambiwa hakuna karatasi ngumu za kutoa leseni hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |