• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Benki Kuu ya Kenya (CBK) yaendelea kuwakumbusha wakenya kubadilisha noti za zamani za Sh1,000

    (GMT+08:00) 2019-09-12 19:53:05
    Benki Kuu ya Kenya (CBK) inazidi kuwahamasisha na kuwakumbusha wakenya kuhusu kukaribia kwa tarehe ya mwisho ya kubadilishwa kwa noti za zamani za Sh1,000 na zile mpya.

    Katika ujumbe uliowekwa kwenye akaunti ya Twitter ya CBK, benki hiyo ilikariri kuwa baada ya tarehe hiyo, noti zote za zamani hazitatumika tena.

    Aidha katika ujumbe huo kwenye mtandao wa Twitter,CBK imetoa wito kwa wakenya kuwakumbusha wazee wanaoishi vijijini kubadilisha pesa za zamani kabla makataa.

    Inaaminika kuwa watu wazima katika jamii za Kiafrika hupenda kuhifadhi pesa katika nyumba zao. Hii ndio maana asasi hii ambayo husimamia sekta ya benki imetoa wito huu.

    Wakati huohuo CBK imekuwa ikitoa wito huo kila siku kupitia matangazo yaliyolipiwa katika magazeti ya kila siku yanayochapishwa humu nchini, redio na runinga.

    Katika jumbe hizo umma hukumbushwa kuhusu siku ambazo zimesalia kabla ya muda wa matakataa uliowekwa kutamatika.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako