• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Yanga yajiongezea mzigo mzito, Malindi yaonja joto ya jiwe

    (GMT+08:00) 2019-09-16 09:01:21
    Mchezo wa kwanza hatua ya Kwanza kwenye kombe la Shirikisho kwa kikosi cha Azam FC dhidi ya Triangle United umeongezeka uzito kwa wawakilishi wa Tanzania baada ya kupoteza mchezo huo.

    Bao pekee la Triangel United ya Zimbabwe lilifungwa dakika ya 34 na Ralph Kawondera kutokana na uzembe wa safu ya ulinzi wa Azam FC. Sasa Azam ina kazi nzito ya kwenda kutafuta matokeo ugenini kwenye mchezo wa marudiano unaoatarajiwa kuchezwa kati ya Septemba 27-29 nchini Zimbabwe.

    Huko Zanzibar nako, wawakilishi wa visiwani humo Malindi SC imeshindwa kutumia vyema fursa ya kucheza nyumbani baada ya kuchapwa mabao 4-1 na Al Masry ya Misri katika mchezo wa kwanza wa raundi ya pili ya kombe la Shirikisho Afrika uwanja wa Amaan, Zanzibar.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako