Bao pekee la Triangel United ya Zimbabwe lilifungwa dakika ya 34 na Ralph Kawondera kutokana na uzembe wa safu ya ulinzi wa Azam FC. Sasa Azam ina kazi nzito ya kwenda kutafuta matokeo ugenini kwenye mchezo wa marudiano unaoatarajiwa kuchezwa kati ya Septemba 27-29 nchini Zimbabwe.
Huko Zanzibar nako, wawakilishi wa visiwani humo Malindi SC imeshindwa kutumia vyema fursa ya kucheza nyumbani baada ya kuchapwa mabao 4-1 na Al Masry ya Misri katika mchezo wa kwanza wa raundi ya pili ya kombe la Shirikisho Afrika uwanja wa Amaan, Zanzibar.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |