Wanasoka wa Russia, Pavel Mamaev na Alexander Kokorin jana wameruhusiwa kutoka gerezani baada ya kukaa jela kwa takribani mwaka mmoja kutokana na kupatikana na hatia ya kushambulia usiku wakati wakiwa wamelewa.
Shirika la habari la Russia limeripoti kuwa klabu ya Zenit St. Petersburg tayari imesaini mkataba mpya na Kokorin. Mkurugenzi wa klabu hiyo, Alexander Medvedev amesema waliamua kusaini mkataba na mchezaji huyo ambao utaisha mwezi Mei mwakani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |