Mukura Victory Sports ndio mabingwa wa mwaka huu wa mashindano ya Agaciro baada ya kuichapa Rayon Sports 2-1 kwenye fainali iliyofanyika uwanja wa Amahoro nchini Rwanda.
Kipigo hicho cha kushtua kwa Rayon Sports kinaizuia timu hiyo kutwaa kombe hilo, timu hizo zilimaliza zikiwa pungufu baada ya wachezaji wao kulimwa kadi nyekundu.
Nayo Polisi wamemaliza wakiwa washindi wa tatu baada ya kuifunga APR kwa goli 1-0.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |