Akizungumza na washiriki wa mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (Tatoa) jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Biashara wa NBC, Elvis Ndunguru amesema mkopo huo utaanzia Sh1 milioni hadi Sh300 milioni.
Amesema mkopo wa bima wa NBC ni maalumu kwa ajili ya bima za biashara zote zikiwemo magari, bidhaa zilizo safarini, majanga ya moto, ujambazi, hatari za barabarani na ajali kwa wafanyakazi.
Mkurugenzi huyo amesema uamuzi wa kuanzisha huduma hiyo inayowalenga wafanyabiashara umetokana na kasi ya utendaji wa serikali ikiwemo kuondoa kero zilizokuwa zikiizorotesha sekta ya uchukuzi nchini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |