Ufichuzi huo uko katika ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka huo ambayo ilikuwa ikikaguliwa na Kamati ya Bunge kuhusu Uwekezaji (PIC).
Kamishna Mkuu wa KRA James Mburu ambaye alifika mbele ya kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Mvita Abdulswamad Nassir alisema kufikia sasa mamlaka hiyo imekusanya Sh112 milioni kati ya fedha hizo ambazo zimejilimbikiza kwa miaka minne.
Bw Mburu aliwaambia wabunge hao kwamba KRA sasa imeweka mikakati murwa ya kuimarisha kiwango cha ukusanyaji ushuru mwingi.
Bw Mburu aliwataja wafanyakazi kadha ambao wameshtakiwa kwa kukwepa kulipa mabilioni ya fedha kama ushuru, ishara ya kujitolea kwa KRA kukusanya ushuru zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |