Hivi sasa China imekuwa nchi ya pili iliyowekeza zaidi katika utafiti duniani, ikiifuata Marekani. Idadi ya watafiti wa China imeshika nafasi ya kwanza duniani kwa miaka sita mfululizo, huku idadi ya makala za sayansi na teknolojia na mara za kunukuliwa zikishika nafasi ya pili duniani. Idadi ya maombi ya hakimiliki za uvumbuzi ya China imeshika nafasi ya kwanza duniani kwa miaka minane.
China siku zote inashikilia uvumbuzi na kuzidi kuimarisha ulinzi wa hakimiliki za ujuzi. Kutokana na uwezo mubwa ya utafiti wa sayansi na teknolojia, teknolojia mpya na bidhaa mpya zinatolewa siku hadi siku, na uchumi wa China unaweza kuendelea kudumisha maendeleo ya kasi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |