Waziri wa mazingira ya ikolojia wa China Bw. Li Ganjie amesema katika miongo saba iliyopita tangu Jamhuri ya Watu wa China ianzishwe, shughuli za kulinda mazingira ya ikolojia nchini China zimepata mafanikio makubwa ya kihistoria na kushuhudia mageuzi ya kihistoria.
Bw. Li pia amesema China imeshiriki kwenye usimamizi wa mazingira duniani na kuwa nchi ya kwanza kutoa mpango wa China wa kutekeleza ajenda ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030 na pia kuongoza mchakato wa mazungumzo kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa duniani, na kuwa mshiriki, mchangiaji na mwongozaji wa ujenzi wa ustaarabu wa ikolojia duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |