• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SportPesa kufunga kampuni zake Kenya kutokana na ushuru wa juu

    (GMT+08:00) 2019-09-30 20:18:07
    Kampuni ya SportPesa imefunga shughuli zake nchini Kenya na hatua ambayo imeona maelfu ya wafanyikazi wao wakienda nyumbani.

    Kampuni za kamare, ambazo zinadhibiti zaidi ya asilimia 60 ya sehemu ya soko nchini Kenya, zimesema wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya ushuru mkubwa uliowekwa na serikali ambao umefanya biashara hiyo kuwa haina faida tena.

    SportPesa, ambayo hapo awali ilionyesha kwamba ilikuwa inarudi kwenye biashara, sasa inasema imesikitishwa na uamuzi wa wabunge wa Kenya wa kutoza ushuru wa asilimia 20 kwa tuzo zote za kamare.

    Kufungwa kwa kampuni za kamare itanyima serikali mapato ya kodi karibu na sifuri na itasimamisha uwekezaji wote katika michezo nchini Kenya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako