• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kampala Benki ya Afrexim kufungua tawi lake Afrika Mashariki mwezi Oktoba

    (GMT+08:00) 2019-09-30 20:18:07
    Benki ya Afrika ya mauzo ya nje na uangizaji imetia saini ya makubaliano na Uganda, ambayo itaona mkopeshaji wa uwekezaji akifungua ofisi yake ya tawi la Afrika Mashariki huko Kampala.

    Mpango huo ulisainiwa na Rais Yoweri Museveni na Benedict Oramah, Rais wa Afrexim. Tawi hilo kampala litakuwa la tano kwa benki hiyo, baada ya Cairo, Abuja, Abidjan na Harare.

    Mkataba huo pia unahakikisha Afrexim na maafisa wake wakuu kinga ya diplomasia katika shughuli nchini Uganda.

    Tawi la Kampala litafunguliwa kwa biashara mwishoni mwa mwezi Oktoba na litahudumia nchi 11: Kenya, Uganda, Sudan, Eritrea, Djibouti, Ethiopia, Sudani Kusini, Tanzania, Rwanda, Burundi na Comoros.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako